-
1 Samweli 28:7-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Hatimaye Sauli akawaambia watumishi wake: “Nitafutieni mwanamke anayewasiliana na roho,+ nitaenda kwake kumwomba ushauri.” Watumishi wake wakamwambia: “Tazama! Kuna mwanamke anayewasiliana na roho kule En-dori.”+
8 Kwa hiyo Sauli akaficha sura yake, akavaa mavazi mengine na kwenda kwa mwanamke huyo usiku akiwa na wanaume wake wawili. Akasema: “Tafadhali, nifanyie uaguzi* kwa kuwasiliana na roho,+ nipandishie yule nitakayekutajia.” 9 Hata hivyo, mwanamke huyo akamwambia: “Unajua vizuri mambo ambayo Sauli alifanya, jinsi alivyowaondoa nchini watu wanaowasiliana na roho na pia wabashiri.+ Kwa nini basi unajaribu kunitega ili niuawe?”+ 10 Ndipo Sauli akamwapia kwa jina la Yehova, akisema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, hutakuwa na hatia yoyote kuhusu jambo hili!” 11 Basi mwanamke huyo akamuuliza: “Nikupandishie nani?” Akajibu: “Nipandishie Samweli.”
-