13 “Waambie Waisraeli, ‘Mnapaswa hasa kushika sabato zangu,+ kwa maana ni ishara kati yangu pamoja nanyi katika vizazi vyenu ili mjue kwamba mimi, Yehova, ninawatakasa ninyi.
8 Ni lazima umtakase kuhani,+ kwa sababu ndiye anayetoa mkate wa Mungu wenu. Mnapaswa kumwona kuwa mtakatifu, kwa sababu mimi, Yehova, ninayewatakasa ninyi, ni mtakatifu.+
23 Mungu wa amani na awatakase kikamili. Na bila kasoro yoyote, roho na nafsi* na mwili wenu akina ndugu, na vihifadhiwe bila lawama wakati wa kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo.+
13 Hata hivyo, tuna wajibu wa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu akina ndugu mnaopendwa na Yehova,* kwa sababu tangu mwanzo Mungu aliwachagua+ ili mwokolewe kwa kuwatakasa+ kupitia roho yake na imani yenu katika kweli.