-
2 Mambo ya Nyakati 2:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Sasa ninajenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu, ili niitakase kwake, nifukize uvumba wenye manukato+ mbele zake, na pia kwa ajili ya mikate ya tabaka* inayotolewa daima+ na pia dhabihu za kuteketezwa, asubuhi na jioni,+ nyakati za Sabato,+ miezi mipya,+ na kwenye majira ya sherehe+ za Yehova Mungu wetu. Huu ni wajibu wa kudumu kwa Waisraeli.
-
-
Nehemia 10:32, 33Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Pia, tukajiwekea wajibu kwamba kila mmoja wetu atoe sehemu ya tatu ya shekeli* kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya* Mungu wetu,+ 33 kwa ajili ya mkate wa tabaka,*+ toleo la nafaka la kila siku,+ dhabihu za kawaida za kuteketezwa za Sabato+ na miezi mipya,+ na kwa ajili ya sherehe rasmi,+ kwa ajili ya vitu vitakatifu, kwa ajili ya dhabihu za dhambi+ ili kufunika dhambi za Waisraeli, na kwa ajili ya kazi zote za nyumba ya Mungu wetu.
-