18 Kwa hiyo Yehova akamwambia Musa: “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mwanamume aliye na roho, na uweke mikono yako juu yake.+ 19 Kisha umsimamishe mbele ya kuhani Eleazari na mbele ya watu wote, nawe umweke kuwa kiongozi.+ 20 Utampa sehemu ya mamlaka yako,+ ili Waisraeli wote wamsikilize.+