Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 18:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Hutakuwa na urithi katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu ya* ardhi miongoni mwao.+ Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.+

  • Hesabu 18:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kwa maana nimewapa Walawi sehemu ya kumi ambayo Waisraeli wananitolea mchango, mimi Yehova, ili iwe urithi wao. Ndiyo sababu nimewaambia, ‘Hawapaswi kuchukua urithi miongoni mwa Waisraeli.’”+

  • Kumbukumbu la Torati 10:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Ndio maana Lawi hana fungu wala urithi pamoja na ndugu zake. Yehova ndiye urithi wake, kama Yehova Mungu wako alivyokuwa amemwambia.+

  • Kumbukumbu la Torati 14:28, 29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 “Mwishoni mwa kila miaka mitatu mnapaswa kuleta sehemu yote ya kumi ya mazao yenu ya mwaka huo na kuyahifadhi ndani ya majiji yenu.+ 29 Kisha Mlawi, ambaye hana fungu wala urithi kati yenu, mkaaji mgeni, yatima, na mjane aliye ndani ya majiji yenu atakuja kula na kushiba,+ ili Yehova Mungu wenu awabariki katika mambo yote mnayofanya.+

  • Yoshua 13:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Musa hakuwapa watu wa kabila la Lawi urithi.+ Urithi wao ni dhabihu zinazochomwa kwa moto zinazotolewa kwa Yehova Mungu wa Israeli,+ kama alivyowaahidi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki