-
Mambo ya Walawi 7:33-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Mguu wa kulia utakuwa fungu la mwana wa Haruni atakayetoa damu ya dhabihu za ushirika na mafuta.+ 34 Kwa maana nachukua kidari cha toleo la kutikiswa na mguu wa lile fungu takatifu kutoka kwa dhabihu za ushirika za Waisraeli na kumpa kuhani Haruni na wanawe. Ni sheria ya kudumu kwa Waisraeli.+
35 “‘Hilo ndilo fungu lililotengwa kwa ajili ya makuhani, yaani, Haruni na wanawe, kutoka katika dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto, fungu lililotengwa kwa ajili yao siku waliyowekwa rasmi kumtumikia Yehova wakiwa makuhani.+
-