12 Mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu,+ ninyi na wana wenu, binti zenu, watumwa wenu wa kiume na wa kike, na Mlawi yeyote aliye ndani ya majiji* yenu, kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+
10 Akawaambia: “Nendeni mkale vitu bora* na kunywa vitu vitamu, na muwapelekee mafungu ya vyakula+ wale ambao hawana chochote; kwa maana hii ni siku takatifu kwa Bwana wetu, nanyi msihuzunike, kwa maana shangwe ya Yehova ndiyo ngome* yenu.”
17 Basi watu wote wa kutaniko waliokuwa wamerudi kutoka utekwani wakajenga vibanda nao wakakaa katika vibanda hivyo, kwa maana Waisraeli hawakuwa wamefanya hivyo tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mpaka siku hiyo, basi wakashangilia sana.+
18 Hili ndilo jambo ambalo nimeona ni jema na linafaa: kwamba mtu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yote ngumu+ anayofanya kwa jasho chini ya jua katika siku chache za maisha alizopewa na Mungu wa kweli, kwa maana hiyo ndiyo thawabu yake.*+