-
Mathayo 19:3-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Mafarisayo wakaja wakikusudia kumjaribu Yesu, wakamuuliza: “Je, ni halali mwanamume kumtaliki mke wake kwa sababu yoyote ile?”+ 4 Akawajibu: “Je, hamkusoma kwamba yule aliyewaumba tangu mwanzo aliwaumba mwanamume na mwanamke+ 5 na kusema: ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?+ 6 Basi wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo, kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.”+ 7 Wakamuuliza: “Basi, kwa nini Musa aliagiza kutoa cheti cha kumfukuza na kumtaliki?”+ 8 Akawajibu: “Musa aliwaruhusu kuwataliki wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu,+ lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo.+
-