-
Marko 10:2-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Mafarisayo wakaja, wakikusudia kumjaribu, wakamuuliza kama ni halali kwa mwanamume kumtaliki mke wake.+ 3 Akawajibu: “Musa aliwapa amri gani?” 4 Wakasema: “Musa aliruhusu kumwandikia cheti cha kumfukuza na kumtaliki.”+ 5 Lakini Yesu akawaambia: “Aliwaandikia amri hiyo+ kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.+ 6 Hata hivyo, tangu mwanzo wa uumbaji ‘Aliwaumba mwanamume na mwanamke.+ 7 Kwa sababu hiyo, mwanamume atamwacha baba yake na mama yake,+ 8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja,’+ basi wao si wawili tena, bali mwili mmoja. 9 Kwa hiyo, kile ambacho Mungu ameunganisha, mtu yeyote asikitenganishe.”+ 10 Walipoingia tena ndani ya nyumba wanafunzi wakaanza kumuuliza kuhusu jambo hilo. 11 Akawaambia: “Yeyote anayemtaliki mke wake na kumwoa mwingine anafanya uzinzi+ dhidi yake, 12 na ikiwa mwanamke baada ya kumtaliki mume wake anaolewa na mwingine, anafanya uzinzi.”+
-