Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 17:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Andika jambo hili katika kitabu liwe ukumbusho,* na uliseme tena kwa Yoshua: ‘Nitawaangamiza kabisa Waamaleki kutoka chini ya mbingu, nao hawatakumbukwa tena.’”+

  • 1 Samweli 14:47, 48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 47 Sauli akauimarisha ufalme wake juu ya Waisraeli, akapigana na maadui wake wote waliomzunguka, alipigana na Wamoabu,+ Waamoni,+ Waedomu,+ wafalme wa Soba,+ na Wafilisti;+ na mahali popote alipoenda aliwashinda. 48 Alipigana kwa ushujaa na kuwashinda Waamaleki+ na kuwaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa waporaji.

  • 1 Samweli 15:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kisha Samweli akamwambia Sauli: “Yehova alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Waisraeli,+ sasa sikiliza anavyosema Yehova.+ 2 Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa sababu waliwapinga Waisraeli walipokuwa njiani wakipanda kutoka Misri.+ 3 Sasa, nenda uwashambulie Waamaleki+ na kuwaangamiza+ wao pamoja na vitu vyao vyote. Usiwaache hai;* unapaswa kuwaua,+ wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanaonyonya, ng’ombe dume na kondoo, ngamia na pia punda.’”+

  • 1 Mambo ya Nyakati 4:42, 43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Baadhi ya watu wa kabila la Simeoni, wanaume 500, walienda kwenye Mlima Seiri+ wakiwa na Pelatia, Nearia, Refaya, na Uzieli, wana wa Ishi ambao waliwaongoza. 43 Kisha wakawaangamiza Waamaleki+ waliobaki ambao walikuwa wametoroka, nao wamekuwa wakiishi huko mpaka leo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki