- 
	                        
            
            1 Samweli 14:47, 48Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
47 Sauli akauimarisha ufalme wake juu ya Waisraeli, akapigana na maadui wake wote waliomzunguka, alipigana na Wamoabu,+ Waamoni,+ Waedomu,+ wafalme wa Soba,+ na Wafilisti;+ na mahali popote alipoenda aliwashinda. 48 Alipigana kwa ushujaa na kuwashinda Waamaleki+ na kuwaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa waporaji.
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            1 Samweli 15:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
15 Kisha Samweli akamwambia Sauli: “Yehova alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Waisraeli,+ sasa sikiliza anavyosema Yehova.+ 2 Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa sababu waliwapinga Waisraeli walipokuwa njiani wakipanda kutoka Misri.+ 3 Sasa, nenda uwashambulie Waamaleki+ na kuwaangamiza+ wao pamoja na vitu vyao vyote. Usiwaache hai;* unapaswa kuwaua,+ wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanaonyonya, ng’ombe dume na kondoo, ngamia na pia punda.’”+
 
 -