-
Yoshua 8:30-32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Kisha Yoshua akamjengea Yehova Mungu wa Israeli madhabahu kwenye Mlima Ebali,+ 31 kama Musa mtumishi wa Yehova alivyowaamuru Waisraeli na kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria+ ya Musa: “Madhabahu ya mawe ambayo hayakuchongwa wala kuguswa na kifaa chochote cha chuma.”+ Na juu yake wakamtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa na pia dhabihu za ushirika.+
32 Kisha akiwa huko akaandika juu ya mawe hayo nakala ya Sheria+ ambayo Musa alikuwa ameandika mbele ya Waisraeli.+
-