-
Hesabu 32:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Musa akawaambia: “Ikiwa mtafanya hivi: Ikiwa mtachukua silaha mbele za Yehova kwa ajili ya vita;+ 21 na ikiwa kila mmoja wenu atachukua silaha na kuvuka Yordani mbele za Yehova anapowafukuza maadui wake kutoka mbele zake+ 22 mpaka mtakaposhinda na kuichukua nchi mbele za Yehova,+ mnaweza kurudi+ nanyi hamtakuwa na hatia mbele za Yehova na Waisraeli. Ndipo Yehova atakapokubali mmiliki nchi hii.+
-
-
Yoshua 22:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Kisha Yoshua akawaita watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase 2 na kuwaambia: “Mmefanya mambo yote ambayo Musa mtumishi wa Yehova aliwaamuru mfanye,+ nanyi mmetii sauti yangu kwa kufanya mambo yote niliyowaamuru.+ 3 Hamjawaacha ndugu zenu kwa muda wote huo, mpaka leo hii;+ nanyi mmetimiza wajibu wa kushika amri ya Yehova Mungu wenu.+ 4 Na Yehova Mungu wenu amewapumzisha ndugu zenu kama alivyowaahidi.+ Basi sasa rudini kwenye mahema yenu katika nchi ambayo Musa mtumishi wa Yehova aliwapa ng’ambo ya* Yordani.+
-