16 Siku tatu baada ya kufanya agano pamoja nao, wakasikia kwamba walikuwa majirani wao na waliishi karibu nao. 17 Ndipo Waisraeli wakaanza safari na kufika katika majiji ya watu hao siku ya tatu; na majiji yao yalikuwa Gibeoni,+ Kefira, Beerothi, na Kiriath-yearimu.+
2 Kisha Daudi na wanaume wote waliokuwa pamoja naye wakaondoka kwenda Baale-yuda ili kuleta Sanduku la Mungu wa kweli+ kutoka huko, ambalo mbele yake watu hulisifu jina la Yehova wa majeshi,+ anayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi.+
6 Daudi na Waisraeli wote wakapanda kwenda Baala,+ mpaka Kiriath-yearimu, jiji la Yuda, ili kuleta kutoka huko Sanduku la Mungu wa kweli, Yehova, anayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+ mahali ambapo watu husali katika jina lake.