Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Hawapaswi kuishi katika nchi yenu, wasije wakasababisha mnitendee dhambi. Mkiiabudu miungu yao, kwa hakika itakuwa mtego kwenu.”+

  • Hesabu 33:55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 “‘Hata hivyo, msipowafukuza wakaaji wa nchi hiyo kutoka mbele yenu,+ basi wale mtakaoruhusu wabaki watakuwa kama vibanzi katika macho yenu na kama miiba kwenye mbavu zenu, nao watawasumbua katika nchi mtakayoishi.+

  • Kumbukumbu la Torati 20:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini katika majiji ya mataifa haya, ambayo Yehova Mungu wenu anawapa yawe urithi wenu, hampaswi kuacha hai kitu chochote kinachopumua.+ 17 Mnapaswa kuwaangamiza kabisa, Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ kama Yehova Mungu wenu alivyowaamuru;

  • Yoshua 23:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Lakini mkimwacha na kushikamana na watu wa mataifa haya yaliyobaki+ na kuoana nao+ na kushirikiana nao, 13 mjue kwa hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyafukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mtego wa kuwanasa, nayo yatakuwa mjeledi wa kuwachapa mbavuni+ na miiba machoni mwenu mpaka mtakapoangamia kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.

  • Waamuzi 1:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Waisraeli walipopata nguvu, waliwatumikisha Wakanaani,+ lakini hawakuwafukuza wote.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki