Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:31-33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 “Nitaweka mpaka wenu kuanzia Bahari Nyekundu mpaka bahari ya Wafilisti na kuanzia nyikani mpaka kwenye Mto Efrati;+ kwa maana nitawatia wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, nanyi mtawafukuza kutoka mbele yenu.+ 32 Hampaswi kufanya agano pamoja nao wala na miungu yao.+ 33 Hawapaswi kuishi katika nchi yenu, wasije wakasababisha mnitendee dhambi. Mkiiabudu miungu yao, kwa hakika itakuwa mtego kwenu.”+

  • Kumbukumbu la Torati 7:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Msioane nao kamwe. Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao wala msikubali wana wenu wawaoe mabinti wao.+ 4 Kwa maana watawapotosha wana wenu waache kumfuata Mungu na kuanza kuabudu miungu mingine;+ kisha hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu, naye atawaangamiza upesi.+

  • Yoshua 23:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Lakini mkimwacha na kushikamana na watu wa mataifa haya yaliyobaki+ na kuoana nao+ na kushirikiana nao, 13 mjue kwa hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyafukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mtego wa kuwanasa, nayo yatakuwa mjeledi wa kuwachapa mbavuni+ na miiba machoni mwenu mpaka mtakapoangamia kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.

  • Waamuzi 2:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Nanyi msifanye agano na wakaaji wa nchi hii,+ bomoeni madhabahu zao.’+ Lakini hamkutii sauti yangu.+ Kwa nini hamkutii? 3 Ndiyo maana nilisema, ‘Sitawafukuza kutoka mbele yenu,+ nao watakuwa mtego kwenu,+ nanyi mtashawishiwa kuifuata miungu yao.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki