-
Hesabu 32:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Musa akawaambia: “Ikiwa mtafanya hivi: Ikiwa mtachukua silaha mbele za Yehova kwa ajili ya vita;+ 21 na ikiwa kila mmoja wenu atachukua silaha na kuvuka Yordani mbele za Yehova anapowafukuza maadui wake kutoka mbele zake+ 22 mpaka mtakaposhinda na kuichukua nchi mbele za Yehova,+ mnaweza kurudi+ nanyi hamtakuwa na hatia mbele za Yehova na Waisraeli. Ndipo Yehova atakapokubali mmiliki nchi hii.+
-
-
Hesabu 32:25-29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakamwambia Musa hivi: “Bwana wetu, sisi watumishi wako tutafanya kama unavyotuamuru. 26 Watoto wetu, wake zetu, mifugo yetu, na wanyama wetu wote watabaki hapa katika majiji ya Gileadi,+ 27 lakini sisi watumishi wako tutavuka, kila mwanamume aliyechukua silaha ili kupigana vita mbele za Yehova,+ kama unavyosema bwana wetu.”
28 Basi Musa akampa kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo* za makabila ya Waisraeli amri kuwahusu. 29 Musa akawaambia hivi: “Ikiwa wana wa Gadi na wana wa Rubeni watavuka Yordani pamoja nanyi, yaani, kila mwanamume aliyechukua silaha ili kupigana vita mbele za Yehova, nanyi mshinde na kuchukua eneo hilo, basi mtawapa eneo la Gileadi ili walimiliki.+
-