16 Mtayaangamiza* mataifa yote ambayo Yehova Mungu wenu atayatia mikononi mwenu.+ Msiwahurumie*+ kamwe, nanyi msiabudu kamwe miungu yao,+ kwa sababu jambo hilo litakuwa mtego kwenu.+
3 Sasa, nenda uwashambulie Waamaleki+ na kuwaangamiza+ wao pamoja na vitu vyao vyote. Usiwaache hai;* unapaswa kuwaua,+ wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanaonyonya, ng’ombe dume na kondoo, ngamia na pia punda.’”+
9 Hata hivyo, Sauli na watu wake walimwacha hai* Agagi na kondoo walio bora, ng’ombe, wanyama waliononeshwa, kondoo dume, na vitu vyote vizuri.+ Hawakutaka kuviangamiza. Lakini waliangamiza vitu vyote visivyo na thamani na visivyofaa.