-
Hesabu 23:19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Akisema jambo, je, hatalitenda?
Akinena jambo, je, hatalitimiza?+
-
-
1 Samweli 2:31-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Tazama! Siku zinakuja nitakapokata nguvu zako na za* nyumba ya baba yako, hivi kwamba hakuna mwanamume yeyote wa nyumba yako atakayeishi na kuzeeka.+ 32 Nawe utamwona adui katika makao yangu miongoni mwa mambo yote mema wanayofanyiwa Waisraeli,+ na kamwe hakutakuwa tena na mzee katika nyumba yako. 33 Mwanamume wako ambaye nitamwacha aendelee kutumikia kwenye madhabahu yangu atayadhoofisha macho yako na kukuletea huzuni, lakini idadi kubwa ya watu wa nyumba yako itauawa kwa upanga.+ 34 Na mambo yatakayowapata wana wako wawili, Hofni na Finehasi, yatakuwa ishara kwako: Wote wawili watakufa siku ileile.+
-