Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 23:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Mungu si mwanadamu anayesema uwongo,+

      Wala si binadamu anayebadili nia yake.*+

      Akisema jambo, je, hatalitenda?

      Akinena jambo, je, hatalitimiza?+

  • 1 Samweli 2:31-34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Tazama! Siku zinakuja nitakapokata nguvu zako na za* nyumba ya baba yako, hivi kwamba hakuna mwanamume yeyote wa nyumba yako atakayeishi na kuzeeka.+ 32 Nawe utamwona adui katika makao yangu miongoni mwa mambo yote mema wanayofanyiwa Waisraeli,+ na kamwe hakutakuwa tena na mzee katika nyumba yako. 33 Mwanamume wako ambaye nitamwacha aendelee kutumikia kwenye madhabahu yangu atayadhoofisha macho yako na kukuletea huzuni, lakini idadi kubwa ya watu wa nyumba yako itauawa kwa upanga.+ 34 Na mambo yatakayowapata wana wako wawili, Hofni na Finehasi, yatakuwa ishara kwako: Wote wawili watakufa siku ileile.+

  • Isaya 55:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana kama mvua na theluji inavyomwagika kutoka mbinguni

      Nayo hairudi huko mpaka iiloweshe dunia na kuifanya izae na kuchipuka,

      Na kumpa mbegu mpandaji na mkate yule anayekula,

      11 Hivyo ndivyo neno langu linalotoka katika kinywa changu litakavyokuwa.*+

      Halitarudi kwangu bila matokeo,+

      Bali hakika litatimiza jambo lolote linalonipendeza,*+

      Na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki