Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 19:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kwa kuwa Yonathani mwana wa Sauli alimpenda sana Daudi,+ alimwambia hivi Daudi: “Sauli baba yangu anakusudia kukuua. Tafadhali jihadhari itakapofika asubuhi, nenda mahali pa siri na ujifiche huko.

  • 1 Samweli 20:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Basi Yonathani akamwapisha tena Daudi kwa msingi wa upendo aliokuwa nao kumwelekea, kwa sababu alimpenda kama alivyojipenda mwenyewe.*+

  • 1 Samweli 20:41
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 41 Mtumishi huyo alipoondoka, Daudi akatoka mahali alipokuwa amejificha hapo karibu upande wa kusini. Kisha akaanguka chini kifudifudi na kuinama mara tatu, nao wakabusiana na kulia pamoja, lakini Daudi alilia zaidi.

  • 1 Samweli 23:16-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Sasa Yonathani mwana wa Sauli akaenda kumwona Daudi huko Horeshi, akamsaidia kupata nguvu* katika Yehova.+ 17 Akamwambia: “Usiogope, kwa maana Sauli baba yangu hatakupata; utakuwa mfalme wa Israeli,+ nami nitakuwa wa pili baada yako; na Sauli baba yangu anajua jambo hilo.”+ 18 Kisha wote wawili wakafanya agano+ mbele za Yehova, na Daudi akaendelea kukaa Horeshi, naye Yonathani akaenda nyumbani kwake.

  • Methali 17:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote+

      Naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+

  • Methali 18:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kuna marafiki walio tayari kuangamizana,+

      Lakini kuna rafiki anayeshikamana na mtu kwa ukaribu kuliko ndugu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki