36 Kisha mfalme akamwita Shimei+ na kumwambia: “Jijengee nyumba Yerusalemu, uishi huko; usitoke huko na kwenda mahali pengine popote. 37 Siku utakapotoka na kuvuka Bonde la Kidroni,+ ujue kwa hakika kwamba utakufa. Damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”