Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kwa maana mwamba wao si kama Mwamba wetu,+

      Hata maadui wetu wameelewa hilo.+

  • Zaburi 18:31-42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+

      Na ni nani aliye mwamba isipokuwa Mungu wetu?+

      32 Mungu wa kweli ndiye anayenivisha nguvu,+

      Naye ataifanya njia yangu iwe kamilifu.+

      33 Huifanya miguu yangu iwe kama ya paa;

      Hunifanya nisimame mahali palipo juu.+

      34 Huizoeza mikono yangu kupigana vita;

      Mikono yangu inaweza kuukunja upinde wa shaba.

      35 Wewe hunipa ngao yako ya wokovu,+

      Mkono wako wa kuume hunitegemeza,*

      Na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.+

      36 Unapanua njia kwa ajili ya hatua zangu;

      Miguu yangu haitateleza.*+

      37 Nitawafuatia maadui wangu na kuwapita;

      Sitarudi mpaka watakapoangamizwa kabisa.

      38 Nitawaponda wasiweze kuinuka;+

      Wataanguka chini ya miguu yangu.

      39 Utanipa nguvu kwa ajili ya vita;

      Utawafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+

      40 Utawafanya maadui wangu wanikimbie,*

      Nami nitawakomesha* wale wanaonichukia.+

      41 Wanalilia msaada, lakini hakuna mtu wa kuwaokoa;

      Hata wanamlilia Yehova, lakini yeye hawajibu.

      42 Nitawaponda wawe laini kama mavumbi katika upepo;

      Nitawatupa nje kama matope barabarani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki