-
1 Mambo ya Nyakati 11:15-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Viongozi watatu kati ya wale viongozi 30 walishuka mwambani kwa Daudi, katika pango la Adulamu,+ wakati jeshi la Wafilisti lilipokuwa limepiga kambi katika Bonde la* Refaimu.+ 16 Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome, na kikosi cha wanajeshi Wafilisti kilikuwa Bethlehemu. 17 Kisha Daudi akasema alichotamani: “Laiti ningekunywa maji kutoka katika tangi lililo karibu na lango la Bethlehemu!”+ 18 Ndipo wale mashujaa watatu wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika tangi hilo lililo karibu na lango la Bethlehemu na kumletea Daudi; lakini Daudi akakataa kuyanywa, akayamwaga mbele za Yehova. 19 Akasema: “Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia, kulingana na maoni ya Mungu wangu, kufanya hivyo! Je, ninywe damu ya wanaume hawa waliohatarisha uhai wao?”*+ Kwa maana walihatarisha uhai wao kwenda kuyaleta. Basi akakataa kuyanywa. Hayo ndiyo mambo waliyotenda mashujaa wake watatu hodari.
-