-
2 Samweli 23:13-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Viongozi watatu kati ya wale viongozi 30 walishuka wakati wa mavuno kwenda kwa Daudi katika pango la Adulamu,+ na kikosi* cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la* Refaimu.+ 14 Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome,+ na kituo cha ulinzi cha Wafilisti kilikuwa Bethlehemu. 15 Kisha Daudi akasema alichotamani: “Laiti ningekunywa maji kutoka katika tangi lililo karibu na lango la Bethlehemu!” 16 Ndipo wale mashujaa watatu hodari wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika tangi hilo lililo karibu na lango la Bethlehemu na kumletea Daudi; lakini akakataa kuyanywa, akayamwaga mbele za Yehova.+ 17 Akasema: “Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia, Ee Yehova, kufanya hivyo! Je, ninywe damu+ ya wanaume walioenda kuhatarisha uhai wao?”* Basi akakataa kuyanywa. Hayo ndiyo mambo waliyotenda mashujaa wake watatu hodari.
-