-
1 Mambo ya Nyakati 22:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Tazama! Utazaa mwana+ atakayekuwa mtu wa amani,* nami nitampumzisha kutokana na maadui wake wote wanaomzunguka,+ kwa maana jina lake litakuwa Sulemani,*+ nami nitawapa Waisraeli amani na utulivu katika siku zake.+ 10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu.+ Atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake.+ Nitakiimarisha kabisa kiti cha ufalme wake juu ya Israeli milele.’+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 2:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Sasa ninajenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu, ili niitakase kwake, nifukize uvumba wenye manukato+ mbele zake, na pia kwa ajili ya mikate ya tabaka* inayotolewa daima+ na pia dhabihu za kuteketezwa, asubuhi na jioni,+ nyakati za Sabato,+ miezi mipya,+ na kwenye majira ya sherehe+ za Yehova Mungu wetu. Huu ni wajibu wa kudumu kwa Waisraeli.
-