-
1 Mambo ya Nyakati 28:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Kisha Daudi akampa Sulemani mwana wake ramani ya ujenzi+ wa ukumbi+ na ya nyumba zake, maghala yake, vyumba vyake vya darini, vyumba vyake vya ndani, na nyumba ya kifuniko cha upatanisho.*+ 12 Alimpa ramani ya kila kitu alichoambiwa kupitia mwongozo wa roho kuhusu ujenzi wa nyua+ za nyumba ya Yehova, vyumba vyote vya kulia chakula vilivyoizunguka, hazina za nyumba ya Mungu wa kweli, na hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu;*+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 3:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ huko Yerusalemu juu ya Mlima Moria,+ mahali ambapo Yehova alikuwa amemtokea Daudi baba yake,+ mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi.+ 2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
-