Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na ni nani anayeweza kumjengea nyumba? Kwa maana mbingu na mbingu za mbingu haziwezi kumtosha,+ basi mimi ni nani hivi kwamba nimjengee nyumba isipokuwa iwe mahali pa kufukizia moshi wa dhabihu mbele zake?

  • 2 Mambo ya Nyakati 6:18-21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Lakini Ee Mungu, je, kweli utakaa duniani pamoja na wanadamu?+ Tazama! Mbingu, naam, mbingu za mbingu, haziwezi kukutosha;+ sembuse nyumba hii niliyoijenga!+ 19 Sasa sikiliza sala yangu mimi mtumishi wako na ombi langu la kutaka kibali, Ee Yehova Mungu wangu, sikiliza kilio changu cha kuomba msaada na sala ambayo mimi mtumishi wako ninasali mbele zako. 20 Macho yako na yatazame nyumba hii usiku na mchana, yatazame mahali ambapo ulisema kwamba utaweka jina lako,+ ili usikilize sala ambayo mimi mtumishi wako ninasali kuelekea mahali hapa. 21 Nawe usikilize sihi zangu mimi mtumishi wako za kuomba msaada na sihi za watu wako Waisraeli wanaposali kuelekea mahali hapa,+ nawe usikilize katika makao yako, kutoka mbinguni;+ naam, usikilize na kusamehe.+

  • Nehemia 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 “Wewe peke yako ndiye Yehova;+ uliumba mbingu, naam, mbingu za mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vilivyo juu yake, bahari na vyote vilivyomo. Nawe unavihifadhi vyote hai, na jeshi la mbinguni linakuinamia wewe.

  • Matendo 17:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, akiwa, kama alivyo, Bwana wa mbingu na dunia,+ hakai katika mahekalu yaliyotengenezwa kwa mikono;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki