-
2 Mambo ya Nyakati 6:18-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 “Lakini Ee Mungu, je, kweli utakaa duniani pamoja na wanadamu?+ Tazama! Mbingu, naam, mbingu za mbingu, haziwezi kukutosha;+ sembuse nyumba hii niliyoijenga!+ 19 Sasa sikiliza sala yangu mimi mtumishi wako na ombi langu la kutaka kibali, Ee Yehova Mungu wangu, sikiliza kilio changu cha kuomba msaada na sala ambayo mimi mtumishi wako ninasali mbele zako. 20 Macho yako na yatazame nyumba hii usiku na mchana, yatazame mahali ambapo ulisema kwamba utaweka jina lako,+ ili usikilize sala ambayo mimi mtumishi wako ninasali kuelekea mahali hapa. 21 Nawe usikilize sihi zangu mimi mtumishi wako za kuomba msaada na sihi za watu wako Waisraeli wanaposali kuelekea mahali hapa,+ nawe usikilize katika makao yako, kutoka mbinguni;+ naam, usikilize na kusamehe.+
-