-
2 Wafalme 19:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Lakini sasa, Ee Yehova Mungu wetu, tafadhali tuokoe kutoka mikononi mwake, ili falme zote duniani zijue kwamba wewe peke yako ndiye Mungu, Ee Yehova.”+
20 Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe huu kwa Hezekia: “Yehova Mungu wa Israeli anasema, ‘Nimesikia sala yako+ ambayo umenitolea kumhusu Mfalme Senakeribu wa Ashuru.+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 6:24, 25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 “Na watu wako Waisraeli wakishindwa na maadui kwa sababu ya kuzidi kukutendea dhambi,+ nao warudi na kulitukuza jina lako+ na kusali+ na kukusihi wapate kibali mbele zako katika nyumba hii,+ 25 basi usikie kutoka mbinguni+ na kuwasamehe watu wako Waisraeli dhambi yao na kuwarudisha katika nchi uliyowapa wao na mababu zao.+
-