-
2 Mambo ya Nyakati 6:32, 33Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 “Pia mgeni ambaye si sehemu ya watu wako Waisraeli na ambaye anatoka katika nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu*+ na mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, akija na kusali kuelekea nyumba hii,+ 33 basi usikilize kutoka mbinguni, makao yako, nawe ufanye mambo yote ambayo mgeni huyo anakuomba ufanye, ili watu wote duniani wajue jina lako+ na kukuogopa, kama watu wako Waisraeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba nyumba hii niliyojenga imeitwa kwa jina lako.
-
-
Isaya 56:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Na wageni wanaojiunga nami Yehova ili kunihudumia,
Kulipenda jina langu mimi Yehova+
Na kuwa watumishi wangu,
Wote wanaoishika Sabato na wasioitia unajisi
Na wanaolishika kabisa agano langu,
7 Nitawaleta pia kwenye mlima wangu mtakatifu+
Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.
Dhabihu zao nzima za kuteketezwa na matoleo yao yatakubaliwa kwenye madhabahu yangu.
Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”+
-