Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 9:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 “‘Ikiwa unaishi na mgeni, anapaswa pia kumtayarishia Yehova dhabihu ya Pasaka.+ Anapaswa kuitayarisha kulingana na sheria na utaratibu uliowekwa wa Pasaka.+ Ninyi nyote mtafuata sheria moja, mkaaji mgeni pamoja na mwenyeji wa nchi.’”+

  • Ruthu 1:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini Ruthu akasema: “Usinisihi nikuache, nirudi na kuacha kukufuata; kwa maana mahali utakapoenda nitaenda, na mahali utakapolala usiku hapo ndipo nitakapolala pia. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.+

  • 2 Wafalme 5:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kisha akarudi kwa yule mtu wa Mungu wa kweli,+ yeye na msafara wake wote,* akasimama mbele yake na kusema: “Sasa najua kwamba hakuna Mungu mahali pengine popote duniani isipokuwa Israeli.+ Sasa, tafadhali, pokea zawadi* kutoka kwangu mimi mtumishi wako.”

  • 2 Mambo ya Nyakati 6:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 “Pia mgeni ambaye si sehemu ya watu wako Waisraeli na ambaye anatoka katika nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu*+ na mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, akija na kusali kuelekea nyumba hii,+ 33 basi usikilize kutoka mbinguni, makao yako, nawe ufanye mambo yote ambayo mgeni huyo anakuomba ufanye, ili watu wote duniani wajue jina lako+ na kukuogopa, kama watu wako Waisraeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba nyumba hii niliyojenga imeitwa kwa jina lako.

  • Isaya 56:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Na wageni wanaojiunga nami Yehova ili kunihudumia,

      Kulipenda jina langu mimi Yehova+

      Na kuwa watumishi wangu,

      Wote wanaoishika Sabato na wasioitia unajisi

      Na wanaolishika kabisa agano langu,

       7 Nitawaleta pia kwenye mlima wangu mtakatifu+

      Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.

      Dhabihu zao nzima za kuteketezwa na matoleo yao yatakubaliwa kwenye madhabahu yangu.

      Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”+

  • Matendo 8:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Ndipo akaondoka na kwenda, na tazama! akamwona towashi* Mwethiopia, mwanamume aliyekuwa na mamlaka chini ya Kandake, malkia wa Waethiopia, na ambaye alisimamia hazina yote ya malkia. Alikuwa ameenda Yerusalemu kuabudu,+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki