-
2 Mambo ya Nyakati 14:2-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Asa alitenda yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake. 3 Aliondoa madhabahu za kigeni+ na mahali pa juu, akazivunjavunja nguzo takatifu,+ na kuikata miti mitakatifu.*+ 4 Zaidi ya hayo, aliwaambia watu wa Yuda wamtafute Yehova Mungu wa mababu zao na kushika Sheria na amri. 5 Kwa hiyo aliondoa mahali pa juu na vinara vya uvumba+ katika majiji yote ya Yuda, na chini ya utawala wake ufalme uliendelea kuwa bila usumbufu.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 14:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Kisha Asa akamlilia Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, haijalishi kwako ikiwa wale unaowasaidia ni wengi au hawana nguvu.+ Tusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea* wewe,+ na katika jina lako tumekuja kupigana na umati huu.+ Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu. Usiache mwanadamu anayeweza kufa akushinde.”+
-