-
1 Wafalme 21:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Basi Ahabu akaingia nyumbani mwake, akiwa amesononeka na kuvunjika moyo kwa sababu ya jibu ambalo Nabothi Myezreeli alimpa aliposema: “Sitakupa urithi wa mababu zangu.” Kisha akalala kitandani mwake, akaugeuzia mbali uso wake, na kukataa kula.
-
-
1 Wafalme 21:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Ahabu akamwambia Eliya: “Yaani umenipata, ewe adui yangu?”+ Akajibu: “Nimekupata. ‘Kwa sababu umeazimia* kutenda maovu machoni pa Yehova,+ 21 sasa ninakuletea msiba, nami nitafagia kabisa baada yako na kumwangamiza kila mwanamume* wa Ahabu,+ kutia ndani wasio na uwezo na walio dhaifu katika Israeli.+ 22 Nami nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha+ mwana wa Ahiya, kwa sababu umenikasirisha na kusababisha Waisraeli watende dhambi.’
-