9 Mwishowe wakafika mahali ambapo Mungu wa kweli alikuwa amemwonyesha, Abrahamu akajenga madhabahu hapo na kupanga kuni juu yake. Akamfunga Isaka mwanawe mikono na miguu na kumlaza kwenye madhabahu juu ya zile kuni.+
7 Wana wa Haruni, makuhani, wataweka moto kwenye madhabahu+ na kupanga kuni kwenye moto huo. 8 Wana wa Haruni, makuhani, watapanga vile vipande vya mnyama wa dhabihu+ pamoja na kichwa na mafuta yanayofunika figo juu ya kuni kwenye moto wa madhabahu.