-
2 Mambo ya Nyakati 21:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Na baada ya mambo hayo yote, Yehova akampiga kwa ugonjwa wa matumbo usioweza kupona.+ 19 Wakati fulani baadaye, baada ya miaka miwili kamili kupita, matumbo yake yalitoka nje kwa sababu ya ugonjwa huo, naye akafa alipokuwa akiteseka sana kwa sababu ya ugonjwa huo; na watu wake hawakuwasha moto kwa ajili yake kama ule uliowashwa kwa ajili ya mababu zake.+ 20 Alikuwa na umri wa miaka 32 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 8 huko Yerusalemu. Hakuna mtu yeyote aliyesikitishwa na kifo chake. Basi wakamzika katika Jiji la Daudi,+ lakini si katika makaburi ya wafalme.+
-