7 Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,
Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
8 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+
Leteni zawadi na mwingie katika nyua zake.
9 Mwinamieni Yehova katika mapambo matakatifu;
Tetemekeni mbele zake, dunia yote!
10 Tangazeni miongoni mwa mataifa: “Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia imeimarishwa kabisa, haiwezi kusogezwa.
Atayahukumu mataifa kwa haki.”+
11 Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;
Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;+
12 Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.+
Wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie kwa sauti+
13 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja,
Anakuja kuihukumu dunia.
Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+
Na mataifa kwa uaminifu wake.+