Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 16:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Mwishowe Samweli akamuuliza Yese: “Je, hawa ndio wana wako wote?” Akajibu: “Aliye mdogo zaidi+ ameachwa mpaka sasa; anawalisha kondoo.”+ Kisha Samweli akamwambia Yese: “Mtume mtu akamwite, kwa sababu hatutaketi kula chakula mpaka atakapokuja hapa.” 12 Basi akamtuma mtu amwite, Yese akamleta ndani. Kijana huyo alikuwa mwekundu, mwenye macho yanayovutia, na mwenye sura nzuri.+ Ndipo Yehova akasema: “Simama, mtie mafuta, kwa maana huyu ndiye!”+

  • 1 Samweli 17:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Daudi alikuwa akienda na kurudi kutoka kwa Sauli ili kuchunga kondoo+ wa baba yake huko Bethlehemu.

  • 1 Samweli 25:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Na baada ya Yehova kukufanyia wewe bwana wangu mambo yote mema aliyoahidi na kukuweka kuwa kiongozi wa Israeli,+

  • 2 Samweli 7:8-11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo,+ uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+ 9 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitafanya jina lako liwe maarufu+ kama jina la watu maarufu duniani. 10 Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza tena kama walivyofanya zamani,+ 11 tangu siku nilipowaweka waamuzi+ juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakupumzisha kutokana na maadui wako wote.+

      “‘“Pia, Yehova amekuambia kwamba Yehova atakujengea nyumba.*+

  • Zaburi 78:70, 71
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 70 Alimchagua Daudi+ mtumishi wake

      Na kumtoa katika mazizi ya kondoo,+

      71 Alimwondoa katika kazi ya kuchunga kondoo wanaonyonyesha;

      Akamfanya kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake,+

      Na wa Israeli, urithi wake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki