-
1 Samweli 16:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Mwishowe Samweli akamuuliza Yese: “Je, hawa ndio wana wako wote?” Akajibu: “Aliye mdogo zaidi+ ameachwa mpaka sasa; anawalisha kondoo.”+ Kisha Samweli akamwambia Yese: “Mtume mtu akamwite, kwa sababu hatutaketi kula chakula mpaka atakapokuja hapa.” 12 Basi akamtuma mtu amwite, Yese akamleta ndani. Kijana huyo alikuwa mwekundu, mwenye macho yanayovutia, na mwenye sura nzuri.+ Ndipo Yehova akasema: “Simama, mtie mafuta, kwa maana huyu ndiye!”+
-
-
2 Samweli 7:8-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo,+ uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+ 9 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitafanya jina lako liwe maarufu+ kama jina la watu maarufu duniani. 10 Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza tena kama walivyofanya zamani,+ 11 tangu siku nilipowaweka waamuzi+ juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakupumzisha kutokana na maadui wako wote.+
“‘“Pia, Yehova amekuambia kwamba Yehova atakujengea nyumba.*+
-