Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 12:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Haya ndiyo masharti na sheria ambazo mnapaswa kuwa waangalifu kutekeleza sikuzote mtakazokuwa hai katika nchi ambayo Yehova Mungu wa mababu zenu atawapa mwimiliki.

  • Kumbukumbu la Torati 17:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Atakapoketi kwenye kiti cha ufalme wake, ni lazima ajiandikie kwenye kitabu* nakala ya Sheria hii, kwa kutumia nakala inayowekwa na makuhani Walawi.+

      19 “Anapaswa kubaki nacho, naye lazima akisome sikuzote za maisha yake,+ ili ajifunze kumwogopa Yehova Mungu wake na kushika maneno yote ya Sheria hii na masharti haya kwa kuyatekeleza.+

  • Yoshua 1:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kitabu hiki cha Sheria kisiondoke kinywani mwako,+ ni lazima ukisome kwa sauti ya chini* mchana na usiku ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo;+ ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.+

  • 1 Wafalme 2:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Ni lazima utimize wajibu wako kwa Yehova Mungu wako kwa kutembea katika njia zake na kushika maagizo yake, amri zake, sheria zake,* na vikumbusho vyake kama vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa;+ ndipo utakapofanikiwa* katika kila jambo unalofanya na kila mahali unapogeuka kwenda.

  • 1 Mambo ya Nyakati 28:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nitauimarisha kabisa ufalme wake milele+ ikiwa atazishika kwa dhati amri zangu na sheria zangu,*+ kama anavyofanya sasa.’

  • Zaburi 19:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Maagizo kutoka kwa Yehova ni ya uadilifu, huufanya moyo ushangilie;+

      Amri ya Yehova ni safi, huyafanya macho yang’ae.+

  • Zaburi 19:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Mtumishi wako ameonywa kupitia hizo;+

      Anapozishika anapata thawabu kubwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki