Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 30:17, 18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 “Lakini moyo wenu ukikengeuka+ na kukataa kusikiliza, mshawishiwe na kuiinamia miungu mingine na kuiabudu,+ 18 nawaambia ninyi leo kwamba hakika mtaangamia.+ Hamtaishi kwa muda mrefu katika nchi mnayovuka Yordani ili kuimiliki.

  • Kumbukumbu la Torati 31:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Sasa Yehova akamwambia Musa hivi: “Tazama! Unakaribia kufa,* na watu hawa wataanza kufanya ukahaba wa kiroho pamoja na miungu ya kigeni inayowazunguka katika nchi wanayoenda.+ Wataniacha na kuvunja agano langu+ ambalo nimefanya pamoja nao.+

  • Kumbukumbu la Torati 31:24-26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Mara tu Musa alipomaliza kuandika maneno yote ya Sheria hii katika kitabu,+ 25 Musa akawaamuru hivi Walawi wanaobeba sanduku la agano la Yehova: 26 “Chukueni kitabu hiki cha Sheria+ mkiweke kando ya sanduku+ la agano la Yehova Mungu wenu, nacho kitakuwa ushahidi dhidi yenu mahali hapo.

  • Yoshua 1:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kitabu hiki cha Sheria kisiondoke kinywani mwako,+ ni lazima ukisome kwa sauti ya chini* mchana na usiku ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo;+ ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki