-
2 Mambo ya Nyakati 26:11-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Zaidi ya hayo, Uzia akawa na jeshi lililojihami kwa ajili ya vita. Wanajeshi hao walienda vitani, wakiwa wamepangwa katika vikundi. Walihesabiwa na kuandikishwa+ na mwandishi Yeieli+ na ofisa aliyeitwa Maaseya, chini ya amri ya Hanania, mmoja wa wakuu wa mfalme. 12 Idadi kamili ya viongozi wa koo* waliowaongoza mashujaa hao hodari ilikuwa 2,600. 13 Wanajeshi waliokuwa chini ya amri yao walikuwa 307,500, wanaume waliokuwa tayari kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme kupigana na maadui.+
-