10 Sasa tazama, ndio hawa wanaume wa Amoni, Moabu, na eneo lenye milima la Seiri,+ ambao hukuwaruhusu Waisraeli wawavamie walipotoka nchini Misri. Waligeuka na kwenda mbali nao na hawakuwaangamiza.+ 11 Sasa wanatulipa kwa kuja kutufukuza kutoka katika miliki yako uliyotupatia iwe urithi wetu.+