-
Ezra 9:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Mara tu niliposikia jambo hilo, nikalirarua vazi langu na joho langu lisilo na mikono na kung’oa baadhi ya nywele za kichwa changu na ndevu zangu, nami nikaketi chini kwa mshtuko. 4 Kisha kila mtu aliyehofu* maneno ya Mungu wa Israeli akakusanyika kunizunguka kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa watu waliotoka uhamishoni, nami nilikuwa nimeketi chini kwa mshtuko mpaka wakati wa toleo la nafaka la jioni.+
-
-
Danieli 9:3-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Basi nikageuza uso wangu kumwelekea Yehova Mungu wa kweli, nikimsihi katika sala, pamoja na kufunga+ na kuvaa nguo za magunia na kujimwagia majivu. 4 Nilisali kwa Yehova Mungu wangu, nikaungama na kusema:
“Ee Yehova Mungu wa kweli, Mungu mkuu na Mwenye kuogopesha, unayeshika agano lako na kuwatendea kwa upendo mshikamanifu+ wale wanaokupenda na kushika amri zako,+ 5 tumetenda dhambi na tumekosea na tumetenda uovu na kuasi;+ nasi tumegeuka na kuacha amri zako na sheria* zako.
-