-
Kutoka 2:23-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Baada ya muda mrefu,* mfalme wa Misri akafa,+ lakini Waisraeli wakaendelea kulia kwa uchungu kwa sababu ya utumwa na kupaza kilio cha malalamishi, na kilio chao cha kuomba msaada kwa sababu ya utumwa kikaendelea kupanda juu kwa Mungu wa kweli.+ 24 Mwishowe Mungu akasikia kilio chao cha uchungu,+ naye akakumbuka agano lake alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.+ 25 Basi Mungu akawakazia uangalifu Waisraeli; na Mungu akayaona mateso yao.
-