-
Kutoka 20:8-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 “Ikumbuke siku ya Sabato na uione kuwa takatifu.+ 9 Fanya shughuli na kazi zako zote kwa siku sita,+ 10 lakini siku ya saba ni sabato kwa Yehova Mungu wako. Usifanye kazi yoyote, wewe wala mwana wako wala binti yako wala mtumwa wako wala kijakazi wako wala mnyama wako wa kufugwa wala mgeni aliye katika makazi* yako.+ 11 Kwa maana kwa siku sita mimi, Yehova, niliumba mbingu na dunia, bahari, na vitu vyote vilivyomo, nami nikaanza kupumzika siku ya saba.+ Ndiyo sababu mimi Yehova niliibariki siku ya Sabato na kuifanya kuwa takatifu.
-
-
Kumbukumbu la Torati 5:12-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 “‘Ishike siku ya Sabato na uione kuwa takatifu, kama mimi Yehova Mungu wako nilivyokuamuru.+ 13 Fanya shughuli na kazi zako zote kwa siku sita,+ 14 lakini siku ya saba ni sabato kwa Yehova Mungu wako.+ Usifanye kazi yoyote,+ wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala kijakazi wako, wala ng’ombe dume wako, wala punda wako, wala mnyama yeyote unayemfuga, wala mgeni anayekaa katika majiji*+ yenu, ili mtumwa wako na kijakazi wako wapumzike kama wewe.+
-