-
Nehemia 10:35-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Pia tutaleta kwenye nyumba ya Yehova mazao ya kwanza yaliyokomaa ya nchi yetu na matunda ya kwanza yaliyoiva ya kila mti wa matunda, mwaka baada ya mwaka,+ 36 vilevile tutatoa wazaliwa wetu wa kwanza wa kiume na pia wa mifugo yetu—kama ilivyoandikwa katika Sheria+—wazaliwa wetu wa kwanza wa ng’ombe na wa kondoo. Tutawaleta kwenye nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani wanaohudumu kwenye nyumba ya Mungu wetu.+ 37 Pia, unga wetu wa kwanza ambao haujakobolewa,+ michango yetu, matunda ya mti wa kila aina,+ divai mpya, na mafuta,+ tutawapelekea makuhani kwenye maghala* ya nyumba ya Mungu wetu,+ pia tutawapa Walawi sehemu ya kumi ya mazao ya mashamba yetu,+ kwa maana Walawi ndio wanaokusanya sehemu za kumi za mazao katika miji yetu yote ya kilimo.
-