8 Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Mimi mwenyewe nilikuweka usimamie michango ninayoletewa.+ Nimekupa wewe na wanao sehemu ya vitu vyote vitakatifu vinavyotolewa kama mchango na Waisraeli ili viwe posho yenu ya kudumu.+
11 Vitu hivi pia vitakuwa vyenu: zawadi ambazo Waisraeli wanatoa kuwa mchango+ pamoja na matoleo yao yote ya kutikiswa.+ Nimekupa wewe na wanao na mabinti wako vitu hivyo ili viwe posho yenu ya kudumu.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.+
13 Je, hamjui kwamba watu wanaofanya kazi takatifu hula vitu vya hekalu, na kwamba wale wanaohudumu kwa kawaida kwenye madhabahu hupata fungu lao kutoka kwenye madhabahu?+