28 “‘Lakini kitu chochote ambacho mtu anamtolea Yehova bila masharti,* iwe ni mwanadamu au mnyama au shamba lake, hakiwezi kuuzwa au kununuliwa tena. Kitu chochote kilichowekwa wakfu ni kitakatifu kabisa kwa Yehova.+
11 Vitu hivi pia vitakuwa vyenu: zawadi ambazo Waisraeli wanatoa kuwa mchango+ pamoja na matoleo yao yote ya kutikiswa.+ Nimekupa wewe na wanao na mabinti wako vitu hivyo ili viwe posho yenu ya kudumu.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.+
26 “Unapaswa kuwaambia hivi Walawi: ‘Mtapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao ili iwe urithi wenu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova mchango wa sehemu ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi.+