Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Unapaswa kuleta katika nyumba yangu mimi, Yehova Mungu wako, mazao bora ya kwanza yaliyokomaa* ya ardhi yako.+

      “Usimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.+

  • Mambo ya Walawi 27:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 “‘Lakini kitu chochote ambacho mtu anamtolea Yehova bila masharti,* iwe ni mwanadamu au mnyama au shamba lake, hakiwezi kuuzwa au kununuliwa tena. Kitu chochote kilichowekwa wakfu ni kitakatifu kabisa kwa Yehova.+

  • Mambo ya Walawi 27:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “‘Kila sehemu ya kumi+ ya mazao ya ardhi au matunda ni mali ya Yehova. Sehemu hiyo ni takatifu kwa Yehova.

  • Hesabu 18:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Vitu hivi pia vitakuwa vyenu: zawadi ambazo Waisraeli wanatoa kuwa mchango+ pamoja na matoleo yao yote ya kutikiswa.+ Nimekupa wewe na wanao na mabinti wako vitu hivyo ili viwe posho yenu ya kudumu.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.+

  • Hesabu 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Unapaswa kuwaambia hivi Walawi: ‘Mtapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao ili iwe urithi wenu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova mchango wa sehemu ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki