Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 14:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na asifiwe Mungu Aliye Juu Zaidi,

      Ambaye amewatia mikononi mwako wale wanaokukandamiza!”

      Na Abramu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote.+

  • Mwanzo 28:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Na jiwe hili ambalo nimelisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu,+ nami sitakosa kukupa sehemu ya kumi ya vitu vyote utakavyonipa.”

  • Hesabu 18:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “Ona kwamba nimewapa wana wa Lawi kila sehemu ya kumi+ katika Israeli iwe urithi wao kwa sababu ya utumishi wao, utumishi wa hema la mkutano.

  • Hesabu 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Unapaswa kuwaambia hivi Walawi: ‘Mtapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao ili iwe urithi wenu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova mchango wa sehemu ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi.+

  • Kumbukumbu la Torati 14:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya mazao ya shambani yanayotokana na mbegu zenu mwaka baada ya mwaka.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 31:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Mara tu agizo hilo lilipotolewa, Waisraeli walitoa kwa wingi mazao ya kwanza ya nafaka, divai mpya, mafuta,+ na asali, na mazao yote ya shambani;+ walileta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+

  • Nehemia 13:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Na watu wote wa Yuda wakaleta kwenye maghala sehemu ya kumi+ ya nafaka, divai mpya, na mafuta.+

  • Malaki 3:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Leteni ghalani sehemu yote ya* kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ tafadhali, nijaribuni kwa njia hii,” asema Yehova wa majeshi, “mwone kama sitawafungulia malango ya mbinguni ya mafuriko+ na kuwamwagia baraka hivi kwamba hamtakosa chochote.”+

  • Luka 11:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Lakini ole wenu Mafarisayo, kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga,+ lakini mnapuuza haki na kumpenda Mungu! Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine.+

  • Waebrania 7:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Ni kweli, kulingana na Sheria, wazao wa Lawi+ ambao hupokea cheo chao cha ukuhani, wana amri ya kukusanya sehemu za kumi kutoka kwa watu,+ yaani, kutoka kwa ndugu zao, ingawa hao ni wazao wa* Abrahamu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki