26 “Unapaswa kuwaambia hivi Walawi: ‘Mtapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao ili iwe urithi wenu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova mchango wa sehemu ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi.+
5 Mara tu agizo hilo lilipotolewa, Waisraeli walitoa kwa wingi mazao ya kwanza ya nafaka, divai mpya, mafuta,+ na asali, na mazao yote ya shambani;+ walileta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+
10 Leteni ghalani sehemu yote ya* kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ tafadhali, nijaribuni kwa njia hii,” asema Yehova wa majeshi, “mwone kama sitawafungulia malango ya mbinguni ya mafuriko+ na kuwamwagia baraka hivi kwamba hamtakosa chochote.”+
42 Lakini ole wenu Mafarisayo, kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga,+ lakini mnapuuza haki na kumpenda Mungu! Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine.+
5 Ni kweli, kulingana na Sheria, wazao wa Lawi+ ambao hupokea cheo chao cha ukuhani, wana amri ya kukusanya sehemu za kumi kutoka kwa watu,+ yaani, kutoka kwa ndugu zao, ingawa hao ni wazao wa* Abrahamu.