-
Nehemia 10:37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
37 Pia, unga wetu wa kwanza ambao haujakobolewa,+ michango yetu, matunda ya mti wa kila aina,+ divai mpya, na mafuta,+ tutawapelekea makuhani kwenye maghala* ya nyumba ya Mungu wetu,+ pia tutawapa Walawi sehemu ya kumi ya mazao ya mashamba yetu,+ kwa maana Walawi ndio wanaokusanya sehemu za kumi za mazao katika miji yetu yote ya kilimo.
-
-
Nehemia 12:44Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
44 Siku hiyo wanaume waliwekwa ili kusimamia maghala+ ya michango,+ mazao ya kwanza,+ na sehemu za kumi.+ Kutoka katika mashamba ya majiji walipaswa kukusanya kwenye maghala hayo mafungu yaliyoamriwa na Sheria+ kwa ajili ya makuhani na Walawi,+ kwa maana kulikuwa na shangwe huko Yuda kwa sababu ya makuhani na Walawi waliokuwa wakihudumu.
-