-
Esta 3:2-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Watumishi wote wa mfalme waliokuwa katika lango la mfalme walikuwa wakimwinamia na kumsujudia Hamani, kwa maana mfalme alikuwa ameamuru atendewe hivyo. Lakini Mordekai alikataa kumwinamia au kumsujudia. 3 Basi watumishi wa mfalme waliokuwa katika lango la mfalme wakamuuliza Mordekai: “Kwa nini unapuuza amri ya mfalme?” 4 Ingawa siku baada ya siku walimuuliza hivyo, hakuwasikiliza. Kisha wakamjulisha Hamani ili kuona kama tabia ya Mordekai ingevumiliwa;+ kwa maana Mordekai alikuwa amewaambia kwamba yeye ni Myahudi.+
5 Sasa Hamani alipoona kwamba Mordekai amekataa kumwinamia na kumsujudia, alikasirika sana.+
-