- 
	                        
            
            1 Wafalme 19:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
3 Basi Eliya akaogopa, akaondoka na kukimbia ili kuokoa uhai wake.*+ Akafika Beer-sheba,+ jiji la Yuda,+ akamwacha mtumishi wake huko. 4 Akaingia nyikani safari ya siku moja, akafika na kuketi chini ya mti wa mretemu, naye akaomba afe. Akasema: “Imetosha! Sasa, Ee Yehova, niue,*+ kwa sababu mimi si bora kuliko mababu zangu.”
 
 -