Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 30:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Kwa maana ninajua kwamba utanishusha katika kifo,

      Katika nyumba ambamo watu wote walio hai watakutana.

  • Zaburi 49:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Anaona kwamba hata watu wenye hekima hufa;

      Wapumbavu na wasiotumia akili huangamia pamoja,+

      Nao hulazimika kuwaachia wengine mali zao.+

  • Zaburi 49:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Lakini mwanadamu, ingawa anaheshimiwa, hataendelea kuishi;+

      Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.+

  • Mhubiri 8:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kama vile ambavyo hakuna mtu aliye na nguvu juu ya roho* au anayeweza kuizuia roho, vivyo hivyo hakuna yeyote aliye na nguvu juu ya siku ya kufa.+ Kama vile ambavyo hakuna yeyote anayeruhusiwa kurudi nyumbani wakati wa vita, vivyo hivyo uovu hautawaruhusu wale wanaozoea kuutenda waponyoke.*

  • Mhubiri 9:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Wote huwa na mwisho uleule,*+ waadilifu na waovu,+ watu wema na safi na wale wasio safi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa dhabihu. Mtu mwema ni sawa na mtenda dhambi; mtu anayeapa ni sawa na yule anayejihadhari kuhusu kuapa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki