-
1 Wafalme 19:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Basi Eliya akaogopa, akaondoka na kukimbia ili kuokoa uhai wake.*+ Akafika Beer-sheba,+ jiji la Yuda,+ akamwacha mtumishi wake huko. 4 Akaingia nyikani safari ya siku moja, akafika na kuketi chini ya mti wa mretemu, naye akaomba afe. Akasema: “Imetosha! Sasa, Ee Yehova, niue,*+ kwa sababu mimi si bora kuliko mababu zangu.”
-
-
Yona 4:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Basi akasali hivi kwa Yehova: “Ee Yehova, je, sikujua utafanya jambo hili nilipokuwa katika nchi yangu? Ndiyo sababu tangu awali nilijaribu kukimbilia Tarshishi;+ kwa maana nilijua kwamba wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema, hukasiriki upesi, una upendo mwingi mshikamanifu,+ na unahuzunishwa na msiba. 3 Sasa, Ee Yehova, nakusihi uniue, kwa maana afadhali nife badala ya kuishi.”+
-